Wednesday, 18 March 2015

MWANAFUNZI WA UDSM ALIYEJIRUSHA KUTOKA GHOROFA YA TATU AVUNJIKA MFUPA WA BEGA





Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam, Cecilia Mosh (26) aliyejirusha kutoka ghorofa ya tatu hadi chini kutokana na hofu ya moto uliotokea katika Hosteli ya Mabibo, amevunjika mfupa wa bega. 

Mwanafunzi huyo alijirusha kupitia dirisha juzi katika harakati za kujiokoa na moto baada ya jengo la wasichana, Block B kushika moto “Nilisikia kelele za moto nikiwa chumbani na nilipotpka nje nikakuta moshi umetanda kila kona, baada ya kuona hivyo nilionona ni vema nijioke kwa kujirusha kutoka ghorofa ya tatu ya bweni hilo hadi chini kupitia dirishani” amesema Cecilia Mosha.