Wednesday, 18 March 2015

JK: BAADHI YA MA-DC WAMETEMWA KWA ULEVI NA MADENI.





Dodoma. Raisi Jakaya Kikwete amesema baadhi ya wakuu wa wilaya walitemwa kutokana na upungufu, ikiwa ni pamoja na madeni mitaani. Rais alisema baadhi yao walikuwa wakienda baa wanalewa na ili kuwaondoa ilibidi wake zao waitwe kuwachunguza.


Raisi Kikwete alisema hayo jana mjini Dodoma alipokuwa akifungua semina elekezi kwa wakuu wa wilaya 27 wapya walioteuliwa hivi karibuni. February 18 mwaka huu, Raisi kikwete alifanya mabadiliko ya wakuu wa wilaya na kutengua uteuzi wa wakuu wa wilaya 12.

Raisi kikwete alisema walikuwepo wenye upungufu na wengine walikuwa na madeni mitaani huku baadhi yao wakiwa na tatizo la ulevi kiasi kwamba wakienda baa hulewa kupita kiasi.

Aliwaasa wakuu wa wilaya wapya kuwa wengine ni wadogo ki-umri lazima wafanane na madaraka waliyopewa.

“Pale ulipo ni role model (mfano wa kuigwa), lazima uwe na tabia njema kwa kauli, matendo, nidhamu na uadilifu usiotiliwa shaka, “alisema Raisi kikwete