Sunday 10 May 2015

NISHA AVAMIWA NA MAJAMBAZI NYUMBANI KWAKE NA KUPORA MALI.


STAA wa filamu za Kibongo, Salma Jabu 'Nisha' usiku wa kuamkia leo amevamiwa na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wapatao watano nyumbani kwake Kijitonyama jijini Dar na kuporwa baadhi ya mali.

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Nisha ameandika kuwa majambazi wapatao watano wakiwa na gari walivamia nyumbani kwake na kumpora huku akimshukuru Mungu maana yeye yuko salama.
Gari la Nisha likiwa limeibiwa baadhi ya vitu.
Staa huyo pia aliweka picha ya gari lake lililokuwa limeibiwa baadhi ya vitu na majambazi hao kisha kuandika hivi:
 

Tukio hili limetokea ikiwa ni siku chache baada ya staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba 'Ali Kiba' naye kuvamiwa na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi wapatao 20 nyumbani kwake Kunduchi, Dar kisha kumpora mali.