Wednesday 20 May 2015

VAN GAAL AWAPIGA MKWARA WASHINDI WA TUZO MAN U

Kocha mkuu wa Klabu ya Manchester United Louis van Gaal amewapiga mkwara mzito wachezaji wake walioibuka na tuzo za msimu za Klabu hiyo huku pia akitoa tahathari kwa wachezaji wote wakubaliane na matokeo ya uongozi utakao amua ni mchezaji gani atabaki na nani ataondoka kwa ajili ya msimu ujao.

Mapema kabla ya utoaji wa tuzo haujachukua mkondo wake, Van Gaal aliwaonya wachezaji wake kutolewa sifa walizozipata kupitia mchakato wa kumsaka mshindi wa tuzo za mwaka na badala yake wanatakia kukaza buti kwa lengo la kufanya vizuri msimu ujao wa ligi.

Amesema ni wakati mzuri kwao kujiapanga kufanya maandalizi ya kutosha wakati wa kujiandaa na msimu wa 2015-16 na ana hakika endapo kila mmoja atawajibiuka kwa nafasi yake Man Utd itafikia malengo ya kutwaa ubingwa.

Hata hivyo ametoa tahadhari ya kufanywa kwa mabadiliko katika sehemu ya kikosi chake, na kuwataka wachezaji kujitayarisha na jambo hilo ambalo litaamuru baadhi yao kuondoka ili wengine kusajiliwa.


Tayari meneja huyo kutoka nchini Uholanzi ameshafikia hatua nzuri ya kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa pembeni wa PSV Eindhoven Memphis Depay.

Tayari mchezaji huyoa meshafanyiwa vipimo vya afya na siku kadhaa zijazo ada yake ya usajili inayotajwa kufikia paund million 25, italipwa ili taratibu nyingine za kusainiwa kwa mkataba baina ya pande hizo mbili zichukue nafasi yake.