Wednesday 20 May 2015

NCHEMBA: WANAFUNZI WAPEWA FEDHA ZAO ZA KUJIKIMU

Bungeni Dodoma leo, Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba, ameiagiza Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kuwalipa Wanafunzi ambao hawajapewa fedha zao za kujikimu hivyo na kusababisha usumbufu kwa wanafunzi hao.

Nchemba aliyasema hayo wakati akitoa taarifa ya muongozo iliyoombwa na Mbunge wa kuteuliwa viti maalumu, Esther Bulayo aliyetaka kujua ni nini kauli ya serikali baada ya wanafunzi zaidi ya elfu 7 wa chuo kikuu cha Dar es Salaam kugoma kushinikiza kupewa fedha zao toka bodi ya mikopo.

Naibu waziri Nchimbi alisimama na kuomba radhi wanafunzi kutokana na usumbufu uliojitokeza, na kusema tayari wizara yake imeshatoa fedha kwa ajili ya malipo kwa wanafunzi wote wa vyuo ambao hawajalpatiwa fedha zao.

”Naagiza vyombo vinavyoshughulikia maswala ya elimu kuwalipa haraka wanafunzi ambao hawajapewa fedha zao ili kuwaepushia usumbufu vyuoni”, alisema Nchimbi .

Jana wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam waligoma kuingia darasani kutokana na kukosa hela za kujikwimu, huku wale wa chuo cha Mtakatifu Joseph nao wakigoma kushinikiza kurudishwa kwa wanafunzi wenzao wa mwaka wa kwanza kurudishwa chuoni baada ya kugoma kutokana na kucheweleshwa kupewa fedha zao toka Bodi ya Mikopo.