Monday 11 May 2015

LULU MICHAEL AFUNGUKA KUWA NA UHUSIANO NA WANAUME WALIOMZIDI UMRI, NDO MPANGO MZIMA KWAKWE.!!


Msanii mrembo na mwenye mvuto katika tasnia ya filamu nchini Tanzania, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa anapenda kuwa na mahusiano na wanaume wanaomzidi umri kwa sababu wanakuwa na nafasi nyingi katika maisha yake.

Akihojiwa amesema kuwa anapenda kuwa na wanaume wanaomzidi kwa sababu wana nafasi tatu katika maisha yake ya kawaida, hazo ni kuwa kama kaka, baba na mpenzi.


Ameongeza kuwa hawezi kuwa na mwanaume ambaye wanalingana umri kwa sababu atakuwa hana sifa hizo pia akili zao zitakuwa hazijakomaa na hivyo kushindwa kushauriana katika kufanya vitu vingi vya maendeleo.