Saturday 18 April 2015

WASANII TUNATESWA NA KIDUDU MTU - THEA


MKONGWE kwenye soko la ugizaji Bongo, Salome Urassa ‘Thea’ amefunguka kuwa miaka ya hivi karibuni wasanii hawaishi pamoja kama zamani kwani shetani amewaingilia katikati na kuwatenganisha


Akizungumza na mwanahabari wetu, Thea alisema kipindi cha nyuma wasanii walikuwa waipenda sana kuwa na kundi moja wakakaa pamoja na kuelewana lakini kukatokea kitu ambacho mpaka leo hakieleweki wakasambaratika.“Naamini kuna vitu tulikosea, tunateseka kweli. Tunatakiwa kabisa kumrudia Muumba wetu kwa kuwa hakuna cha Bongo Movies wala nini na ninaona inaelekea kufa kabisa lazima tukae na kujikagua upya,” alisema Thea.

Credit:GPL