Jeshi la polisi Kanda Maalum ya Dar
es Salaam, linaendelea na uchunguzi dhidi ya Mlinzi wa Katibu Mkuu wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo, Dk.Wilbrod Slaa anayedaiwa kufanya njama ya kumuua kwa
sumu, Bw. Khalid Kagezi.
Akizungumza na waandishi wa habari
leo,Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova
amesema wamechukua maelezo kwa Katibu Mkuu Dk.Wilbrod Slaa pamoja na maelezo ya
mlizi wake Khalid Kagezi.
Kamishina Kova amesema Chadema
walichukua hatua mbalimbali na kujiridhisha kuhusika kwa mlinzi wa Dk.Slaa
kufanya mikakati ya kumuua kwa sumu kwa kuiweka katika maji au chakula.
Amesema kwa maelezo ya Mlinzi huyo
alidai kuteswa na baadhi ya watu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo kwa
kuwataja kwa majina.
Kamishina Kova amesema Kagezi alidai
kutekwa na kushambuliwa katika mwili wake na jeshi la Polisi likampa fomu namba
tatu (PF3)kwa ajili ya matibabu
“Jeshi la Polisi limefanya jitihada
kwa kupata maelezo kwa watu wote ambao wamehusika kwa mlizi na Dk.Slaa”amesema
Kamishina Kova.
Amesema baada ya uchunguzi
watapeleka kwa wakili wa serikali