Mshambuliaji
wa Mancity Wilfried Bonny alifunga bao lake la kwanza na kuiweka kifua mbele
Mancity baada Gareth McAuley kupewa kadi nyekundu.
Fernandinho
na David Silva waliongeza mabao mengine mawili na kuisaidia City kupunguza
idadi ya pointi kati yake na viongozi wa ligi Chelsea kuwa tatu hadi pale
kikosi hicho cha Jose Mourinho kitakapocheza mechi zake mbili.
Hatahivyo
mechi hiyo iliangazia sana kutolewa kwa mchezaji McAuley baada ya sekunde 89
pekee,ikiwa ni uamuzi wa mapema sana kufanywa katika ligi ya Uingereza msimu
huu,ilipobainika kwamba refa Neil Swarbrick alitoa kadi nyekundi kwa
mtu ambaye hakustahili.