Tuesday 19 May 2015

SNURA AFUNGUKA KUHUSU SAKATA LA SHILOLE NA BASATA


Wiki iliyopita kulikuwa na vichwa vya habari kuhusu Baraza la Sanaa Taifa kutoa barua ya Onyo kwa msanii Shilole baada ya kuonekana akiwa wazi sehemu za juu ya mwili wake jukwaani kwa bahati mbaya kwenye show yake  aliyoenda kuifanya Ubelgiji.


Shilole na Snura ni watu ambao wanafananishwa na kupambanishwa na wakati mwingine kulinganishwa kwenye muziki wanaoufanya.. millardayo.com imepata nafasi ya kuongea na Snura kuhusu hili lililomtokea Shilole.

Snura ameanza hivi>>’Kiukweli kabla sijataka kusema itakuaje, mimi binafsi kutoka kwenye moyo wangu namuombea sana msamaha na Watanzania wasimuangalie hivyo ambavyo wanamuangalia‘

Sentensi nyingine Snura amesema>>’Ile ni kama ajali hivyo wamuelewe kama ambavyo mwenyewe amesema yule ni mtu mzima na ana maumivu yake ndani ya moyo kwa hiyo unapozidi kumkandamiza ni kama unazidi kumuumiza kikubwa ni kumsamehe na kuona  je itatokea tena?‘