Monday 18 May 2015

SHAMBULIO MAREKANI LAUWA 9

Polisi nchini Marekani wamesema kuwa watu tisa wameuawa katika shambulio lililotekelezwa na watu wenye silaha waliokuwa kwenye pikipiki katika mkahawa mmoja katika mji wa Waco.

Hata hivyo watu wengine 18 walipelekwa hospitali kupatiwa matibabu kutokana shambulio hilo. Maofisa katika mji huo wanasema kuwa walibaini mkusanyiko kati ya watu watano walioonekana kupanga jambo lisilo la kawaida. Watu waliokuwa katika mkahawa huo walijificha katika chumba cha majokofu katika harakati za kujiokoa kabla ya kusaidiwa na Polisi kutoka katika eneo hilo.