Wednesday 20 May 2015

JK:WANAOIPONDA SHIRIA YA MITANDAO :CYBER CRIME" WALETE MAPENDEKEZO YAO

Rais wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, amesema dhana ya uwazi katika kuwahudumia wananchi isiwe kwa taasisi za serikali peke yake, bali pia hata kwa asasi za kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali.

Rais wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, amesema dhana ya uwazi katika kuwahudumia wananchi isiwe kwa taasisi za serikali peke yake, bali pia hata kwa asasi za kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo kwa pamoja yana jukumu la kuwahudumia Watanzania.

Akizungumza katika mkutano wa kimataifa wa ubia katika uwazi serikalini, Rais Kikwete amesema inashangaza kuona jamii inakuwa na mtazamo potofu pale serikali inapozitaka asasi za kiraia kuweka wazi utendaji wake, kwani amesema hatua hiyo itasaidia kuondoa mashaka waliyonayo wananchi juu ya utendaji wa asasi hizo.

Rais ametolea mfano wa matumizi mabovu ya rasilimali zinazokwenda kwa asasi za kiraia na kwamba dhana ya uwazi ni muhimu hasa kipindi hiki ambapo kiasi kikubwa cha misaada na pesa za wahisani zinazoletwa nchini zinapitia kwa asasi za kiraia.

Aidha, Rais Kikwete pia amezungumzia pia sheria ya makosa ya mitandao ambayo ameisaini hivi karibuni na kusema kuwa uwepo wa sheria hiyo itakuwa ni mkombozi kwa wahanga wa matukio ya uhalifu unaofanywa kupitia mitandao.


Rais Kikwete amewataka watu wote ikiwa ni pamoja na mashirika ya kimataifa na asasi za kiraia kutoikosoa sheria hiyo, bali kupeleka mapendekezo yao mahali husika ili yafanyiwe kazi kwa ajili ya maboresho ya sheria hiyo