Mwanafunzi wa Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam , Cecilia Mosha (26) aliyejirusha kutoka ghorofa ya
tatu hadi chini kutokana na hofu ya moto uliotokea katika Hosteli ya Mabibo,
amevunjika mfupa wa bega. Mwanafunzi huyo alijirusha kupitia dirishani juzi
katika harakati za kujiokoa na moto baada ya jengo la wasichana, Block A
kushika moto.
" Nilisikia kelele za moto nikiwa chumbani na nipotoka nje nikakuta moshi umetanda kila kona, baada ya kuona hivyo niliona ni vema nijiokoe kwa kujirusha kutoka ghorofa ya tatu ya bweni hilo hadi chini kupitia dirishani,” amesema Cecilia Mosha.
Alisema baada ya kuruka hadi chini alikimbizwa katika kituo kidogo cha
afya karibu na hosteli hiyo ambako alipoteza fahamu na kushtukia yupo katika
Taasisi ya Mifupa (MOI).