Thursday, 19 March 2015

UPDATE NEWS: AJALI NYINGINE YA BASI YATOKEA MIKUMI LEO


Basi la Luwinzo na basi ndogo la Masanga Line Express zimepata ajali kwa kugonga katika hifadhi ya Mikumi barabara kuu ya Iringa-Morogoro na kusababisha watu saba kupoteza maisha papo hapo huku wengine 17 wakijeruhiwa katika tukio lililotokea leo majira ya saa 6 mchana mkoani Morogoro.

Ajali hiyo ni ya pili ndani ya siku mbili baada ya ajali nyingine katika hifadhi hiyo ikihusisha basi la FM Safari na Fuso kutokea marchi 17 majira ya saa 5:30 asubuhi na kusababisha watu wawili kufariki dunia na wengine nane kujeruhiwa.



Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paulo alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo kimetokana na utelezi ukichangiwa na mwendo kasi hali iliyomfanya dereva wa basi ndogo la Msanga Line Express kushindwa kulimudu vyema gari na kwenda kuligonga basi la Luwinzo lililokuwa likitokea Njombe kuelekea Dar es Salaam.