Friday 29 May 2015

YOUNG THUG AMCHOKOZA TENA LIL WAYNE

Kulingana na taratibu za kisheria, rapper Young Thug alilazimika kubadilisha jina la his last album “ Carter 6” kwenda “Barter 6” kwa sababu tayari lilikwisha tumika na bosi wa young money Lil wayne kama mtiririko wa album zake. 
Taarifa ikufikie kwamba Thug ameweka wazi kulirudia jina hilo, katika mixtape yake inayofuata na sasa hivi ataipa jina la “The Carter V”

Akifunguka kupitia kipindi cha radio cha “No days off”, Young Thug amesema ameamua kulitumia jina hilo kwa kuwa Lil wayney ameshindwa kutoa “The Carter V”.

“I’ma drop one more mixtape [before my album] I’ll probably name it Tha Carter V, ’cause the original Carter V still ain’t came out yet. I don’t know what the fu*k they doing. So I’ma put that motherfu*ker out for ’em.” Alisema Thug.

Chokochoko hii inaibuka ikiwa ni miezi miwili imepita, tangu wakali hawa wawili waingie kwenye bifu zito lililosababishwa na matumizi ya jina “Carter 6”.