ISSA MNALLY/Amani11
HAJAKOMA? Staa wa Bongo Fleva anayesumbua na wimbo wa Chumvini, Khaleed Mohamed ‘TID’ amehusishwa na msala mwingine baada ya kudaiwa ku kumjeruhi James Richard, mkazi wa Jiji la Dar.
HAJAKOMA? Staa wa Bongo Fleva anayesumbua na wimbo wa Chumvini, Khaleed Mohamed ‘TID’ amehusishwa na msala mwingine baada ya kudaiwa ku kumjeruhi James Richard, mkazi wa Jiji la Dar.
.
Khaleed Mohamed ‘TID’.
Alisema
wakati anashambuliwa na TID, Dulla aliwaambia watu waliokuwepo kuwa wasiamulie
na ambaye angekaidi angemchoma kisu cha chembe ambapo waliogopa mpaka alipofika
mjumbe wa mtaani huo, akaamulia.
Alisema kuwa
TID alimpiga kiasi ambacho uso ulivimba, kuteguliwa mkono na kuchomwa visu
kichwani na kisogoni ambako alitokwa damu nyingi hadi wasamaria wema
walipoungana na mjumbe kumsaidia kisha kumkimbiza Kituo cha Polisi cha
Oysterbay damu zikiwa zinamtoka chapachapa ambako alipata hati ya polisi ya
matibabu (PF3) na kufungua kesi iliyosomeka OB/RB/3211/2013.
Kitendo
hicho kiliwakasirisha polisi waliokuwa zamu ambapo mmoja wao alisema
anamshangaa TID kurudia kosa lililompeleka gerezani huko nyuma.James alisema
baada ya kufungua kesi hiyo, alikimbizwa katika Hospitali ya CCBRT ambako
alishonwa nyuzi nne katika jeraha la kisogoni na kupatiwa dawa kwa ajili ya
maumivu ya mkono na usoni ambako alivimba sana.
“Leo naenda
(Jumanne) naenda tena hospitali ili nijaziwe PF3 yangu kwa ajili ya kulipeleka
shauri hili mahakamani,” alisema James kwa masikitiko.Jitihada za kumpata TID
anayesakwa na jeshi la polisi ili kusikia kauli yake kuhusiana na madai hayo
hazikuzaa matunda kufuatia simu yake kutopatikana hewani.
Hata hivyo, waandishi wetu wanaendelea kumtafuta.
Hata hivyo, waandishi wetu wanaendelea kumtafuta.
Chanzo: GPL